Eugenius wa Karthago

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake iliyoko Milano, Italia.

Eugenius wa Karthago (alifariki 13 Julai 505) alikuwa Mkristo aliyechaguliwa kwa kauli moja kuwa askofu wa mji huo mwaka 480 baada ya Deogratias wa Karthago (aliyefariki 456).

Ilimbidi atetee imani sahihi kwa kupambane na Uario, ulioungwa mkono na mfalme wa Wavandali. Alifaulu kuwavuta baadhi yao katika Kanisa Katoliki na kwa sababu hiyo alifukuzwa akaishi uhamishoni katika jangwa la Libia [1].

Halafu aliruhusiwa kurudi, lakini miaka minane baadaye akafukuzwa tena ahamie Vienne, karibu na Albi (leo nchini Ufaransa). Huko alijenga monasteri aliposhika maisha ya toba hadi kifo chake[2].

Kutokana na imani na maadili yake, tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 13 Julai[3].

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

  • Expositio Fidei Catholicae
  • Apologeticus pro Fide
  • Altercatio cum Arianis.[4]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. On setting out he wrote a letter of consolation and exhortation to the faithful of Carthage which is still extant in the works of St. Gregory of Tours (P.L., LVII, 769-71)
  2. http://catholicsaints.info/saint-eugene-of-carthage/
  3. Martyrologium Romanum
  4. Cain, Andrew. “Miracles, Martyrs, and Arians: Gregory of Tours' Sources for His Account of the Vandal Kingdom.” Vigiliae Christianae, vol. 59, no. 4, 2005, pp. 412–437. JSTOR website Retrieved 13 July 2019.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.