Ermengol wa Urgell

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ermengaudi)
Mt. Ermengol katika mavazi ya askofu.
Masalia ya Mt. Ermengol.
Wasia wa Mt. Ermengol, Arxiu Comarcal de l'Alt Urgell.

Ermengol wa Urgell (pia: Armengol au Armengod au Hermengaudius; alifariki El Pont de Bar, 1035) alikuwa askofu wa Urgell kuanzia mwaka 1010.

Mtoto wa ukoo tawala[1][2], alianza uaskofu wake kwa kurekebisha maisha ya mapadri wa kanisa kuu kufuatana na mafundisho ya Agostino wa Hippo

Anatajwa kama mhusika wa kuteka mji wa Guissona mwaka 1024 na kuurudisha kwenye Ukristo.

Alishindana mara nyingi na masharifu wa Urgell na kuwajibika katika ujenzi wa miundombinu, likiwemo kanisa kuu la Urgell.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Novemba[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. The Bishop Builds a Bridge: Sanctity and Power in the Medieval Pyrenees, Jeffrey A. Bowman, The Catholic Historical Review, Vol. 88, No. 1 (Jan., 2002), 1-3.
  2. Catalunya Romànica, vol. VII, "La Cerdanya, El Conflent", Enciclopedia Catalana, Barcelona, 1995, p. 265.
  3. Martyrologium Romanum
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.