Chitungwiza

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kituo cha manunuzi Chitungwiza.

Chitungwiza ni mji wa Zimbabwe, kilometa 9 upande wa kusini wa mji mkuu Harare. Mwaka 2022 ulikuwa na wakazi 371,000[1]. Walio wengi wanafanya kazi Harare kwa sababu kuna nafasi chache tu za ajira.

Chitungwiza ilipata cheo cha manispaa mwaka 1981. Asili yake ni mitaa mitatu ya Seke, Zengeza na St Marys iliyojengwa wakati wa ubaguzi wa rangi kama makazi ya Waafrika wasioruhusiwa kukaa Harare penyewe.

Siku hizi Chitungizwa ni mji wa kukua haraka Zimbabwe. Kiwanja cha ndege cha Harare kipo karibu.


Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Chitungwiza kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.