Basiano wa Lodi

Basiano wa Lodi (kwa Kilatini: Bassianus; 310 hivi - Siracusa, Sicilia, Italia, 19 Januari 409) alikuwa askofu wa mji huo wa Italia Kaskazini kuanzia mwaka 373 hadi kifo chake.
Kama kijana alikwenda Roma kwa masomo, na huko aliongokea dini ya Ukristo. Baba yake alitaka aasi na kurudi nyumbani, lakini yeye alikataa na kukimbilia Ravenna.
Baada ya kuchaguliwa askofu, alishiriki mtaguso wa Akwileia (381) na labda hata mtaguso wa Milano (390). Ili kulinda kundi lake dhidi ya uzushi wa Ario, uliokuwa bado na nguvu katika eneo hilo, alipambana kwa bidii pamoja na rafiki yake askofu Ambrosi wa Milano. Pamoja naye alisaini barua kwa Papa Sirisi.
Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Kanisa la Kiorthodoksi kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Januari[1].
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |