Apoloni wa Roma
Mandhari

Apoloni wa Roma (Roma, Italia, karne ya 2 - Roma, 21 Aprili 185) alikuwa mwanafalsafa wa ukoo maarufu ambaye alitetea Ukristo hata kwa maandishi na kwa sababu hiyo aliuawa katika dhuluma ya kaisari Commodus.
Baada ya kuutetea mbele ya gavana Pereni na ya Senati ya Dola la Roma kwa hotuba fasaha, aliuthibitisha ukweli wake kwa ushahidi wa damu yake[1].
Habari zake tumezipata kutoka kwa mwanahistoria Eusebi wa Kaisarea, Jeromu na wengineo[2][3].
Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
- Mababu wa Kanisa
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |