Antoni wa Kiev

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya Mt. Antoni.

Antoni wa Kiev au Antoni Pekerski (kwa Kirusi Антоний Печерский; kwa Kiukraina Антоній Печерський; Liubek, 983 hivi - Kiev, 7 Mei 1073) alikuwa mkaapweke kwenye mlima Athos (Ugiriki) hadi alipotumwa kurudi kwao kueneza umonaki katika sehemu za Kiev (leo nchini Ukraina) zilizopokea Ukristo tangu muda mfupi[1].

Baada ya kuanzisha monasteri kadhaa[2], alirudi upwekeni kwenye mlima Athos hadi alipotumwa tena Kiev ambapo, pamoja na Theodosi wa Kiev alianzisha ile maarufu ya Mapango ya Kiev.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Mei[3] lakini pia tarehe 23 Julai.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.