Alfa na Omega

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Herufi kubwa alfa na omega.

Alfa (Α au α) na omega (Ω or ω) ndizo herufi ya kwanza na ya mwisho ya alfabeti ya Kigiriki.

Kwa sababu hiyo zimechukuliwa kama ishara ya mwanzo na mwisho.

Kitabu cha Ufunuo (1:8, 21:6 na 22:13)[1] kinazitumia pamoja kama jina la Yesu Kristo na la Mungu[2][3], kwa kuwa ndio asili na kikomo cha viumbe vyote.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Katika Uyahudi[hariri | hariri chanzo]

Maandishi ya Uyahudi yanasema kuwa neno emet (אמת, yaani "uaminifu"), moja ya sifa kuu za YHWH, linaundwa na herufi ya kwanza, ya kati na ya mwisho wa alfabeti ya Kiebrania.

Katika Uislamu[hariri | hariri chanzo]

Qur'an (57:3) inataja al'Awwal (الأول), yaani "Wa Kwanza" na al'Akhir (الآخر), yaani "Wa Mwisho" kati ya majina ya Allah.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "Revelation Red". CCEL.org. 
  2. Notes on the New Testament, Explanatory and Practical by Albert Barnes. 1956, 1962, 1974. ISBN 978-0825422003
  3. Gauding, Madonna (2009). The signs and symbols bible : the definitive guide to mysterious markings. New York, NY: Sterling Pub. Co. uk. 84. ISBN 9781402770043. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Alfa na Omega kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.