Ahazi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ahazi katika Promptuarii Iconum Insigniorum, kazi ya Guillaume Rouillé (1553).

Ahazi (kwa Kiebrania אָחָז, ʼAḥaz; kwa Kigiriki: Ἄχαζ, Ἀχάζ, Akhaz; kwa Kilatini: Achaz;[1] kifupisho cha Jehoahaz, יְהוֹאָחָז, Yəhō’aḥaz, Yehō’aḥaz)[2] alikuwa mfalme wa Yuda, mtoto na mrithi wa Yothamu tangu mwaka 732 KK hadi 716 KK[3][4].

Ahazi anachorwa kama mtu mbaya katika Kitabu cha Pili cha Wafalme (16:2), Kitabu cha Isaya 7-9 na Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 28.

Alitabiriwa na nabii Isaya kwamba mwanamwali atamzalia mtoto wa kiume atakayethibitisha uwepo wa Mungu pamoja na watu wake, jina lake Emanueli litakavyomaanisha. (7:1-17) Kweli mke wa Ahazi alimzaa Hezekia atakayeendeleza ufalme wa ukoo wa Daudi, lakini Wakristo wanaona utabiri huo ulimlenga zaidi Yesu, mwana wa Bikira (walivyoelewa watafsiri wa kwanza wa Biblia katika Kigiriki) ambaye kweli ni Mungu pamoja nasi, na ni mwana wa Daudi ambaye atatawala milele kwa amani na haki (11:1-9).

Kwa kukosa imani katika msaada huo wa Mungu Ahazi aliwaita Waashuru na hivyo kuchangia mangamizi ya Ufalme wa Israeli (Kaskazini)[5] .

Injili ya Mathayo inamtaja katika orodha ya vizazi vya Yesu.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Douay-Rheims Catholic Bible, Isaias (Isaiah) Chapter 7.
  2. Hayim Tadmor and Shigeo Yamada, The Royal Inscriptions of Tiglath-pileser III (744-727 BC) and Shalmaneser V (726-722 BC), Kings of Assyria. (The Royal Inscriptions of the Neo-Assyrian Period 1; Winona Lake, IN: Eisenbrauns, 2011), Tiglath-Pileser III 47 r 11'.
  3. Edwin R. Thiele (1994-10-01). The Mysterious Numbers of the Hebrew Kings. Kregel Academic. ISBN 978-0-8254-3825-7. 
  4. William F. Albright has dated his reign to 744 – 728 BC.
  5. "Isaiah 7", Eerdmans Commentary on the Bible, (James D. G. Dunn, John William Rogerson, eds.) 2003, ISBN 9780802837110, p. 505

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

  • Ahaz. JewishEncyclopedia.com.
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ahazi kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.