Adriani wa Canterbury
Adriani wa Canterbury, O.S.B. (alifariki 9 Januari 710) alikuwa mmonaki msomi na hatimaye kwa miaka 39 abati huko Canterbury, Kent, Uingereza.
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Kadiri ya Beda Mheshimiwa, alikuwa Mberberi[2] kutoka Afrika Kaskazini.
Baada ya kuongoza monasteri karibu na Napoli, Papa Vitalian alimteua mara mbili kuwa askofu mkuu wa Canterbury, lakini alikataa akipendekeza wengine.
Theodoro wa Tarso alipokubali, Vitalian alimuagiza Adriani aongozane naye kwenda Britania, kwa sababu alijua njia hadi Galia.
Theodoro alifika huko 669, kumbe Adriani alizuiwa kwa muda, lakini alipofika tu Canterbury alifanywa abati kama Papa alivyokuwa ameagiza.
Adriani akiwa maarufu kwa ujuzi wake wa Biblia, Kigiriki na Kilatini aliowashirikisha wanafunzi wengi[3], [4], pamoja na kuwa kiongozi bora, alifanya monasteri yake kuwa na athira kubwa.[5]
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Martyrologium Romanum
- ↑ Serralda, Vincent; Huard, André (1984-01-01). Le Berbère-- lumière de l'Occident (kwa Kifaransa). Nouvelles Editions Latines. uk. 147. ISBN 9782723302395.
- ↑ Martyrologium Romanum
- ↑ Lapidge, Michael (2006). The Anglo-Saxon Library. Oxford: Oxford UP. ku. 33, 87–88. ISBN 9780199239696.
- ↑ Bede, Historia ecclesiastica gentis Anglorum iv. 1, 2.; and Vita Abbatum Wiramuth., in Smith's Beda, p. 293.; W. Malmes. De Pontif. p. 340.
Marejeo ya Kiswahili
[hariri | hariri chanzo]- John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 15
- Maurice Soseleje, Kalendari yetu – Maisha ya Watakatifu – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Peramiho 1986 – ISBN 9976-63-112-X, uk. 10-11
- Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 11
Marejeo ya lugha nyingine
[hariri | hariri chanzo]- Long, George. The Biographical Dictionary of the Society for the Diffusion of Useful Knowledge. London: Longman, Brown, Green & Longmans, 1842-1844. 4 vols.
- Attwater, Donald and Catherine Rachel John. The Penguin Dictionary of Saints. 3rd edition. New York: Penguin Books, 1993. ISBN 0-14-051312-4.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |