Yosefu Calasanz

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. José de Calasanz, Zaragoza.

Yosefu Calasanz, Sch.P. (kwa Kihispania José de Calasanz; Peralta de la Sal, Aragon, leo nchini Hispania, 11 Septemba 1557 - Roma, Italia, 25 Agosti 1648) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki maarufu kwa kuanzisha shule za bure ili kulea vijana katika upendo na hekima ya Injili[1].

Kwa ajili hiyo huko Roma alianzisha Shirika la Waskolopi lenye kulenga elimu ya watoto maskini.

Alitangazwa na Papa Benedikto XIV kuwa mwenye heri tarehe 7 Agosti 1748, halafu Papa Klementi XIII alimtangaza mtakatifu tarehe 16 Julai 1767.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Josep Domènech i Mira, Joseph Calasanz (1557–1648), "Prospects: Quarterly Review of Comparative Education. Paris, UNESCO, XXVII: 2, 327–39. [1] Archived 24 Septemba 2015 at the Wayback Machine.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.