Esuperansi wa Cingoli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Esuperansi huko Cingoli (karne ya 12).

Esuperansi wa Cingoli (alizaliwa Afrika Kaskazini - alifariki Cingoli, Marche, Italia) alikuwa askofu wa mji huo mwishoni mwa karne ya 5[1].

Tangu zamani anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[2].

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 24 Januari[3].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Mtoto wa familia ya Wamani na Waario, alikubaliwa na baba yake kupata ubatizo katika Kanisa Katoliki akiwa na umri wa miaka 12.

Baada ya kukomaa, aliishi kimonaki na kuinjilisha maeneo ya Afrika Kaskazini.

Alipotaka kuhamia Italia na kufika Roma alikamatwa, lakini Papa alifaulu kumtoa akamfanya askofu wa Cingoli. Huko alifanya kazi miaka 15 hadi kifo chake akiwa na sifa ya kufanya miujiza[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Pius Bonifacius Gams, Series episcoporum Ecclesiae Catholicae (Leipzig: 1931), p. 712.
  2. Our Sunday Visitor's encyclopedia of saints by Matthew Bunson 2003 ISBN|1-931709-75-0 page 307
  3. Martyrologium Romanum
  4. Pásztor, Edith. "Esuperanzio di Cingoli". 

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Francesco Maria Rafaelli, Delle memorie ecclesiastiche intorno l'istoria, ed il culto di santo Esuperanzio antico vescovo, e principal protettore di Cingoli, libri due, in Pesaro: nella stamperia Gavelliana, 1762;
  • Giuseppe Avarucci, Una lamella iscritta: problemi ed ipotesi intorno al culto di s. Esuperanzio a Cingoli, Macerata 1986;
  • Adriano Pennacchioni, Vita di S. Esuperanzio, Vescovo e protettore di Cingoli, Cingoli 1991;
  • Pio Cartechini, Il culto dei santi patroni Esuperanzio e Sperandia in alcuni documenti dell'archivio comunale di Cingoli, in Atti del convegno "Santità femminile nel duecento: Sperandia patrona di Cingoli", Ancona 2001, pp. 269–314;
  • Gianluca Orsola, Esuperanzio di Cingoli. Agiografia di un vescovo medioevale, prefazione di Edith Pásztor, Graphe.it edizioni, Perugia 2009, ISBN 9788889840559

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.