Vostok

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mfano wa chombo cha anga Vostok pamoja na sehemu ya juu ya roketi

Vostok (kwa Kirusi Восто́к, mashariki) ilikuwa jina la mradi wa kwanza wa usafiri wa anga-nje uliofaulu kupeleka binadamu kwenye anga-nje na kuwarudisha tena salama.

Ilikuwa mradi wa Umoja wa Kisovyeti ulioshindana na mradi wa Mercury wa Marekani. Mwanaanga Yuri Gagarin alikuwa binadamu wa kwanza aliyerushwa juu katika chombo Vostok 1 tarehe 12 Aprili 1961 na kuzunguka dunia mara moja katika anga-nje kwa kimo kati ya kilomita 315 na 169.

Mradi wa Vorstok ilikuwa na safari sita za kupeleka wanaanga nje ya angahewa ya Dunia kati ya 1961 na 1963; safari ndefu ilidumu siku tano ambapo Vostok 6 ilimpeleka mwanaanga Valentina Tereshkova aliyekuwa mwanamke wa kwanza katika anga-nje.

Mradi ulitumia roketi za kijeshi zilizobeba chomboanga chenye sehemu mbili

Wakati wa kurudi wanaanga walirushwa kutoka dambra wakarudi ardhini kwa parachuti.