Valentina Tereshkova

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Valentina Tereshkova

Valentina Vladimirovna Tereshkova (Kirusi Валентина Владимировна Терешкова) (* 6 Machi 1937) alikuwa mwanaanga kutoka Umoja wa Kisovieti na mwanamke wa kwanza aliyefika kwenye anga-nje.

Alikuwa mtoto wa mkulima aliyeendelea kusoma uhandisi akafaulu kupita mtihani kwa shule ya wanaanga mwaka 1962.

Tar. 16 Juni 1963 alirushwa kwa chombo cha angani Vostok 6 akazunguka dunia mara 49 akarudi duniani 19 Juni.

Astrowiki.PNG
Mradi wa Astronomia Makala hii imewahi kukaguliwa na kuboreshwa kwenye warsha ya pamoja ya Jenga Wikipedia ya Kiswahili, Wikimedia Community User Group Tanzania na ASSAT. Imepewa hali ya ulinzi. Tunaomba mapendekezo yote ya usahihisho na nyongeza zipelekwe kwanza kwenye ukurasa wa majadiliano