Vita ya Vietnam

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha za vita ya Vietnam

Vita ya Vietnam kati ya miaka 1960 na 1975 ilikuwa vita iliyopigwa katika nchi ya Vietnam lakini mapigano yake yalienea hadi nchi jirani za Kambodia na Laos. Wakati ule Vietnam iligawiwa katika madola mawili ya Vietnam Kusini na Vietnam Kaskazini.

Kwa upande mmoja walisimama serikali ya Vietnam Kusini pamoja na askari za Marekani na nchi mbalimbali zilizoshikamana nao; kwa upande mwingine wanamgambo wa Vietkong pamoja na jeshi la Vietnam Kaskazini iliyosaidiwa na nchi za Kikomunisti kwa pesa na silaha.

Mapigano yalitokea hasa ndani ya Vietnam Kusini. Vietnam Kaskazini ilishambuliwa kwa mabomu ya ndege ya Marekani na wanajeshi wake walitumwa kupiga vita katika kusini.

Vita ilikwisha kwa ushindi wa Vietnam kaskazini mwaka 1975.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vita ya Vietnam kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.