United People's Democratic Party

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

United People's Democratic Party (UPDP) ni chama cha siasa nchini Tanzania kilichosajiliwa rasmi tarehe 4 Februari 1993.

Katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 chama hakikumsimamisha mgombea wa kiti cha urais na badala yake kilimuunga mkono mgombea wa chama cha National Convention for Construction and Reform-Mageuzi (NCCR-Mageuzi) kilichomsimamisha Sengondo Mvungi ambaye alipata asilimia 0.49% ya kura zote

Katika uchaguzi wa mwaka 2015 kilimsimamisha Fahmi Dovutwa kama mgombea wa urais.[1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Dovutwa survives road accident", Daily News, 25 October 2015. Retrieved on 2020-09-10. Archived from the original on 2016-06-16.