Ufalme wa Nkore

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Ufalme wa Nkore
Ramani ya Uganda (rangi ya pinki) kuonesha eneo (rangi nyekundu) ulipokuwa Ufalme wa Nkore.

Ufalme wa Nkore (kwa Runyankore; kwa Kiingereza: Ankole) ulikuwa himaya ya kitamaduni za Kibantu huko Uganda. Himaya hiyo ilikuwa inapatikana upande wa Kusini Magharibi mwa Uganda, Mashariki mwa Ziwa Edward. Himaya hiyo ilikuwa ikitawaliwa na serikali iliyojulikana kama vile Mugabe au Omugabe.

Watu wake walijulikana kama Banyankole (wakiwa wengi) na Munyankole (akiwa mmoja) hivyo lugha yao ya kibantu ilijulikana kama Runyankole.

Ufalme huo ulikubali ulinzi wa Uingereza tarehe 25 Oktoba 1901[1]. Ulifutwa rasmi mwaka 1967 chini ya utawala wa serikali ya rais Milton Obote na haujarudishwa rasmi.[2]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "The Ankole Agreement 1901". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-01-12. Iliwekwa mnamo 2020-09-20. 
  2. [http://web.archive.org/20071203235759/http://www.ugandaobserver.com/new/archives/2005arch/features/interview/apr/int200503311.php Archived 3 Desemba 2007 at the Wayback Machine. The Observer Media Ltd. :: The Weekly Observer :: Uganda's Top Resource site
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ufalme wa Nkore kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.