Sakristia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sakristia ikiwa na mavazi yameandaliwa.

Sakristia (kutoka Kilatini "sacristia"; kwa Kiingereza "sacristy") ni chumba maalumu kwa ajili ya kutunza mavazi ya liturujia (kama vile alba na kasula) na vifaa vingine vya ibada za Kikristo (kama vile mkate, divai, mishumaa n.k.).[1]

Kwa kawaida sakristia iko jirani na ukumbi wa kanisa, ili padri na watumishi waingie moja kwa moja baada ya kuvaa kiibada.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "Vestry". English Oxford Living Dictionaries. Oxford University Press. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-11-26. Iliwekwa mnamo 2017-10-14. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: