Nyama choma

Nyama choma ni nyama iliyopikwa kwa kuchomwa kwa moto, makaa au jiko la umeme. Pia nyama inaweza kuchomwa na majiko maalum ya kisasa ya gesi ya kuchomea nyama.
Nyama inaweza ama kuchomwa moja kwa moja, ama kwanza kuchemshwa au kupikwa na moshi, mtindo maarufu hasa Marekani, kabla ya kuchomwa.
Harufu yake inavutia watu wengi kuipenda katika nchi na tamaduni mbalimbali duniani. Hivyo imekuwa biashara hasa katika barabara za mijini.
Nyama hii hupendwa pia wakati wa sherehe, matukio muhimu ya kifamilia na marafiki au mwisho wa wiki kwa wale wanaokunywa pombe. Pamoja na kuliwa na vyakula vingine, mara nyingi huandaliwa na kachumbari.
Tofauti za nyama choma duniani
Afrika ya Mashariki
Nyama choma ni maarufu sana Afrika Mashariki, hasa Tanzania na Kenya. Nyama choma katika nchi hizi huitwa mishikaki.
Afrika Kusini
Huko Afrika Kusini nyama huitwa braai kutokana na neno la Kiafrikana "braaivleis."
Namibia
Nchini Namibia, nyama choma ambayo huitwa kapana huchomwa kwa moto wa kuni. Nyama hii hukatwa vipande vidogo na kuchomwa sio zaidi ya dakika 10. Ni nyama maarufu sana kwenye masoko na sehemu za starehe.
Uswidi
Nchini Uswidi, kuchoma nyama moja kwa moja kwenye makaa ya moto ndio njia maarufu.
Mexico
Kaskazini mwa Mexico, carne asada ni chakula kikuu. Aina maarufu ni pamoja na arrachera, beefsteak na rib eye, pamoja na chorizo. Kuni na makaa hutumiwa.[1]
Argentina na Uruguay
Huko Argentina na Uruguay, asado (nyama iliyochomwa kwenye moto wa wazi) na a la parrilla (nyama ya ng'ombe iliyochomwa kwenye jiko la asili) ni moja ya chakula kikuu.
Japani

Kwenye miji ya nchini Japani, mikokoteni ya yakitori, migahawa au madukani, nyama chomwa huuzwa. Nyama iliyolainishwa kwa marinadi huchomwa kwenye jiko la mkaa kwa kutumia vijiti. Huko Malaysia, Singapore, Indonesia, na Thailand, nyama choma iitwayo satay, ambayo ni nyama iliyolainishwa na kuchomwa kwa makaa kisha huliwa na karangawhich is marinated meat on a bamboo skewer grilled over a charcoal fire and served with peanut (sate) sauce.
Athari za kiafya
Utafiti unaonyesha kuwa kuchoma nyama kwa joto la juu kunaweza kusababisha magonjwa mbalimbali.[2][3] Lakini kulainisha nyama kwa kutumia marinadi kunaweza kupunguza hatari ya magonjwa hayo.[4]
Nyama chooma huaminika kuwa njia mbadala bora ya kupika kuliko kutumia mafuta, ingawa uchomaji unaweza kufanya nyama kuwa kavu.[5]
Marejeo
- ↑ Weekends have a carne asada smell to them. Mexico News Network. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-03-20. Iliwekwa mnamo 12 July 2018.
- ↑ Sugimura, Takashi; Wakabayashi, Keiji; Nakagama, Hitoshi; Nagao, Minako (April 2004). "Heterocyclic amines: Mutagens/carcinogens produced during cooking of meat and fish". Cancer Science 95 (4): 290–299. . Archived from the original on 19 June 2010. https://web.archive.org/web/20100619224815/http://scorecard.org/chemical-profiles/summary.tcl?edf_substance_id=50%2d32%2d8. Retrieved 1 February 2015.
- ↑ Chemicals in Meat Cooked at High Temperatures and Cancer Risk - National Cancer Institute. Cancer.gov. Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-12-21. Iliwekwa mnamo 2015-02-01.
- ↑ "Health | Marinating 'may cut cancer risk'", BBC News, 2008-12-30. Retrieved on 2015-02-01. Archived from the original on 2008-12-31.
- ↑ (2012) Sausage & Mash (in en). London: Bloomsbury Publishing, 16. ISBN 9781408187760. Retrieved on 10 February 2017.
Viungo vya nje
- Video ya nyama choma ya mbuzi Tanzania
- Makala ya picha za nyama choma toka sehemu mbalimbali duniani
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Nyama choma kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |