Msambia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Msambia
(Eriobotrya japonica)
Msambia ukichanua
Msambia ukichanua
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Rosales (Mimea kama mwaridi)
Familia: Rosaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mwaridi)
Jenasi: Eriobotrya
Lindl.
Spishi: E. japonica
(Thunb.) Lindl.

Msambia au mplamu wa Japani (Eriobotrya japonica) ni kichaka kikubwa au mti mdogo wa familia Rosaceae. Matunda yake yaliyo matamu au machungu kidogo huitwa masambia. Ikiwa yameiva yana rangi ya manjano.

Asili ya mti huu ni Uchina lakini hutokea pia huko Japani, Korea na milima ya Uhindi na Pakistani. Siku hizi hupandwa duniani kote katika maeneo yasiyo na joto au baridi sana. Katika Afrika ya Mashariki huonekana sana.

Picha[hariri | hariri chanzo]