Mnazi (mti)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mnazi
(Cocos nucifera)
Mnazi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Rosids (Mimea kama mwaridi)
Oda: Arecales (Mimea kama mpopoo)
Familia: Arecaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mpopoo)
Jenasi: Cocos
Spishi: C. nucifera
L.

Mnazi (Cocos nucifera) ni kati ya miti muhimu zaidi kwa ajili ya uchumi wa kibinadamu katika nchi za tropiki.

  • tunda lake laitwa nazi ni chakula
  • nyama ya tunda hukaushwa kuwa nguta (au: mbata). Nguta hutumiwa viwandani kwa kutengeneza mafuta ya kulika.
  • utomvu ni kinywaji chenye afya kwa sababu ya vitamini yake
  • utomvu uliochachuka "mnazi" ni kinywaji cha pombe
  • ubao unatumiwa kwa ujenzi wa nyumba au jahazi
  • majani kwa paa za nyumba, mikeka au makofia.
  • Mafuu ya mbegu hutumiwa kama kuni au kutengeneza vifaa vya muziki au urembo kama vile bandili, hereni au mikufu.

Mnazi ni mmea wa familia ya Palmae (au: Arecaceae). Asili yake inafikiriwa iko Asia ya kusini lakini umesambaa tangu karne nyingi sana. Mbegu wake unaweza kuzaa hata baada ya kukaa kwenye maji ya bahari kwa muda fulani hivyo inawezekana ya kwamba mnazi ulisambaa peke yake kwenye pwani za bahari. Lakini bila shaka watu waliibeba safarini kwa sababu ni chakula.


Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]