Nazi (tunda)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ya mnazi na tunda lake la nazi
Nyuzi zinaondolewa katika ganda la nazi (Sri Lanka)
Kutengeneza mikeka kutoka nyuzi za nazi (Sri Lanka)
Nazi mtini zikiiva

Nazi ni tunda la mbegu la mnazi. Ina ganda la nje, ganda ngumu au mfuu wa ndani, nyama ya mbegu na utomvu ndani ya uwazi wa mbegu.

Ina matumizi mengi katika maisha ya binadamu.

Nyama ya mbegu[hariri | hariri chanzo]

  • Nyama ya mbegu wake yake huliwa bichi.
  • Nyama iliyokauka huitwa nguta (au: mbata). Nguta hutumiwa kwa kutengeneza mafuta ya kulika.

Ganda la mbegu[hariri | hariri chanzo]

  • Ganda la nje ni ya nyuzi nyingi. Zinatumiwa kwa kutengeneza mikeka, kamba na vitu vingi vingine.
  • Ganda la ndani ni ngumu. Hutumiwa nyumbani kama chombo cha kikombe au cha kukorogea chakula. Kutokana na mlio wake likipigwa inatumika kama chombo cha muziki. Hutumiwa pia kama kuni. Inavaa vilevile kwa kutengeneza makaa.

Utomvu[hariri | hariri chanzo]

  • Utomvu ndani ya mbegu ni kinywaji safi na cha afya.
  • Utomvu ukichachuka ni pombe nyepesi inayoitwa "mnazi"
  • Utomvu ni safi kabisa wakati mbegu unafunguliwa hivyo unaweza kusaidia kuongeza damu mwilini mwa mwanadamu kama dawa lenyewe halipo.