Utomvu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Utomvu wa mpira ukikusanywa mtini
Kukusanya utomvu wa mnazi

Utomvu ni kiowevu kinachopitishwa katika seli za mimea. Unasafirisha maji na lishe ndani ya mmea[1].

Kutokana na aina mbili tofauti za seli za mimea, yaani zilemu na floemu, kuna aina mbili za utomvu wa zilemu na utomvu wa floemu[2].

Utomvu wa zilemu[hariri | hariri chanzo]

Utomvu wa zilemu ni mmumunyo wa maji na homoni, madini na lishe nyingine, Mwendo wake ni kutoka mizizi kuelekea kwenye majani.

Utomvu wa floemu[hariri | hariri chanzo]

Utomvu wa floemu ni mmumunyo wa maji na sukari, homoni na madini. Inashuka kutoka sehemu ambako kabohaidreti na sukari zinalishwa kwenda pale zinapohitajika, yaani kwenye sehemu ambako mmea unakua au sehemu ambako kabohaidreti zinatunzwa kama akiba.

Matumizi[hariri | hariri chanzo]

Watu wametumia aina za utomvu, hasa ya floemu, tangu kale.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Sap (plant physiology), tovuti ya Encyclopedia Britannica online
  2. PLANTS AND THEIR STRUCTURE Archived 22 Oktoba 2006 at the Wayback Machine., On-Line Biology Book, 2001
Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Utomvu kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.