Mawasiliano ya simu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mawasilianoanga)

Mawasiliano ya simu (tafsiri ya Kiingereza-Kigiriki "telecommunication" kutoka Kigiriki tele "mbali" na Kiingereza communication "kupeana habari, mawasiliano") ni kazi ya kupeana habari juu ya umbali tofauti na maongezi ya moja kwa moja kati ya watu walio karibu.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Zamani mawasiliano kwa umbali yalitekelezwa kwa msaada wa ngoma maalumu, alama za moto kutoka mlimani au alama za moshi zilizoonekana kwa mbali. Katika historia ya Ulaya au Asia kuna pia mifano ya semafori au heliografi (kioo cha kuakisisha nuru ya jua, kilichowekwa juu ya mnara au mlima).

Inawezakana kutaja hapa pia nyaraka zilizosafirishwa kwa njia ya wakimbiaji au kwa watu waliopanda farasi.

Tangu karne ya 19 mitambo inayotumia umeme imechukua nafasi hiyo kama vile simu, televisheni, redio au intaneti.

Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.