Master Jay

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Joachim Marunda Kimaryo
Jina Kamili Joachim Marunda Kimaryo
Jina la kisanii Rap Master Jay, Master Jay, Baba Nuru nk.
Nchi Tanzania
Alizaliwa 9 Agosti 1973
Aina ya muziki Hip Hop, Bongo Flava, Kwaya, Dansi
Kazi yake Mtayarishaji
Miaka ya kazi 1995 - sasa
Ameshirikiana na P Funk, Bonny Luv,Rajabu Marijani, Bizz Man, Marco Challi nk.
Ala Kinanda,Guitar, Kinakilishi, Kuunjini Sauti
Kampuni MJ Records

Joachim Marunda Kimaryo (maarufu kama Master J; alizaliwa 9 Agosti 1973) ni muandaaji wa muziki nchini Tanzania.

Master J amewahi kupata tuzo ya Kili Music Awards mara mbili, mwaka 2004 na 2006. Master Jay ana uwezo mkubwa sana wa utengenezaji wa muziki. Anamiliki studio tatu tofauti, moja ya muziki wa Kwaya, moja ya Bongo Flava na nyingine ya muziki wa Dansi.

Familia[hariri | hariri chanzo]

Ni mtoto wa kwanza katika familia ya marehemu Sylvan Kimaryo na mama yake, Scholastica Kimaryo, ambaye alikua ni afisa wa UNDP nchini South Africa ambapo dada yake Catherine Kimaryo anaishi nchini Tanzania akiwa mfanyabiashara mwenye kampuni yake Nchanasaa Consulting Limited (NCL).

Elimu[hariri | hariri chanzo]

Master J alipata elimu ya msingi katika shule ya msingi Upanga lakini aliishia darasa la PILI na kuhamishiwa Botswana baada ya familia yake kuhamishiwa nchini huko kikazi.

Mwaka 1996 alipata digrii ya electronics katika chuo cha City University Of London kilichopo bara Ulaya mbali na shughuli za kimuziki.

Muziki na vikwazo vya kifamilia[hariri | hariri chanzo]

Baada ya kupata digrii yake alirudi nyumbani na kuendelea na shughuli zake za kawaida pamoja na muziki, baba yake hakutaka kabisa mwanae ajishughulishe na muziki kiasi kufikia kutaka kumuachia radhi.

Pamoja na vikwazo alivyopewa na baba yake mzazi, Master J hakuacha muziki kwa kudai kuwa umo ndani ya damu yake. Ni Jaji mkali lakini ana hekima ya Solomoni.

Studio rasmi[hariri | hariri chanzo]

Mnamo mwaka 1996 Master Jay aliamua kujishulisha kabisa na masuala ya utengezaji wa muziki kwa kuamua kuanzisha rasmi studio yake aliyoipa jina lake la "MJ Productions" japokuwa babake alikuwa haja ridhia hilo.

Baadae akatoa wimbo wa kundi la Deplowmatz, Kwanza Unit na baada ya muda kidogo tena akatoa nyimbo za kundi la 4 Crews Flavour, baada ya hapo ndipo mzee wake alipoanza kuoynesha moyo na kuanza kukubali Anachofanya na hii ilinipa moyo wa kufanya kazi kwa bidii zaidi.


Makala hii kuhusu mwanamuziki/wanamuziki fulani wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Master Jay kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.