Majadiliano ya mtumiaji:Muzney Muhammad

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Karibu kwenye Wikipedia kwa Kiswahili!

Tunamfurahia kila mmoja anayeingia na kuungana nasi. Hii ni kamusi elezo ya maandishi huru. Unaweza kuandika makala uipendayo ama kuitafsiri kutoka Wikipedia ya lugha nyingine.

Ukipenda kutumia kurasa zetu za mwongozo na msaada, a) ukitumia simu bofya kwa "Dawati" chini kwenye dirisha lako na n) ubadilishe mwonekano wa Wikipedia kwa kubofya "Switch to old look" kwenye menyu upande wa kushoto.

Kwa mawili matatu labda tazama:

Jisikie huru kuuliza swali lolote lihusianalo na Wikipedia hii. Karibu kujitambulisha kwenye "Ukurasa wa mtumiaji". Ukitaka kupata kwanza uzoefu wa kuweza kuhariri Wikipedia, tafadhali tumia ukurasa wako kwa majaribio. Humo unaruhusiwa kujipatia uzoefu wa uundaji wa makala za Wikipedia! Juu yako mwenyewe uandike tu kwenye ukurasa wako wa mtumiaji. Humo uko huru kutangaza chochote upendacho, kama si biashara au matusi.

Ujue miiko:

Tunakushauri pia kuandikisha email yako; haitaonekana na wengine lakini wataweza kukuandikia kupitia mfumo wa Wikipedia. Karibu sana!


Welcome to Kiswahili Wikipedia!

We welcome you even if you don't speak Kiswahili. For a bot flag go to this site. If you try to edit entries as a non-speaker, it is better to first communicate with one of our admins who can advise you. You may find them at Wikipedia:Wakabidhi. And, please:

  • do not post computer translated texts (like Google Translate, Content Translation, etc. all do not work for Swahili)
  • nor copied texts/images from other webs to this site!
  • do not use links to commercial pages, never post anything that looks like advertising.

As a newcomer we advise that you register your email. This will not be visible to others but it allows us to notify you, which often is helpful in case of problems.

Hongera kwa makala kuhusu utamaduni wa Kiajemi! Kipala (majadiliano) 16:10, 8 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

Ndugu, asante kwa michango yako juu ya Uislamu wa Kishia. Hata hivyo, angalia nilivyoirekebisha ili usirudie makosa yaleyale, kama vile kutafsiri kurasa za Kiingereza kama zinavyoonekana badala ya kutumia chanzo chake, kutafsiri maelezo ya picha ambazo hazionekani katika Kiswahili kwa sababu iliyotangulia, kuongeza katika mabano maneno ya sifa yasiyotakiwa katika kamusi elezo n.k. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:53, 21 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
Shukran,mimi Bado najifunza kutumia wikipedia, Kuna kirasa nyingi natamani kuzitafsiri ila Bado shida kubwa ninayoipata ni hiyo ya kutumia chanzo sijajua ni wapi natakiwa niweke chanzo cha ukurasa niliotafsiri. Naomba msaada wenu 41.222.181.212 17:51, 21 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
Ahsante Muzney Muhammad (majadiliano) 06:29, 22 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
Ukurasa wowote wa Wikipedia unaonyesha juu kabisa maneno "Hariri chanzo". Ukibonyeza utaona chanzo ambacho unaweza kukifanyia kazi. Hapo, kwa mfano, hata picha zitaonekana katika tafsiri yako. Kazi njema! Wote tumejifunza polepole. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:01, 22 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
Haya ahsante 41.222.181.212 12:23, 22 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

Hakimili za makala zako[hariri chanzo]

Ndugu nimeona sasa kwamba michango yako ni tafsiri ya sentensi kwa sentensi kutoka https://en.wikishia.net/view/Usul_al-Din. Sina uhakika kama hii inaruhusiwa tukizingatia kanuni za Wikipedia:Hakimiliki. Kwa hiyo nimeweka makala ya Misingi ya Dini/Usul-din kwa sasa kwenye orodha ya makala kwa ufutaji nikaomba majadiliano tufanyeje. Pamoja na hayo, matini ilhali inatokea kwenye tovuti ya kidhehebu haifai sana kwa ajili ya Wikipedia. Nakupa "Pole" kwa kazi unayofanya maana kuonyesha mafundisho ya Kishia hapa Swwiki ina maana! Ningependekeza utumie makala za en-wikipedia (ziko nyingi kuhusu Uislamu) ambako uko huru kupanusha sehemu juu ya mafundisho ya Kishia. Ila tu hata kama Mkatoliki anachangia kuhusu mafundisho ya kikatoliki, si sawa kutumia lugha inayodokeza mafundisho hayo ni "ya kikristo" kama madhehebu mengine yanatofautiana; ni sawa kabisa kuionyesha kama mafundisho ya kikatoliki. Hivyo ndivyo jinsi tunavyotakiwa kuandika kuhusu dini nyingine pia, hapa tukiweza kutambua tofauti zilizopo. Kipala (majadiliano) 18:56, 23 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

Shukran Kwa mawazo, ila sijaelewa vizur tatizo lililopo ni kuandika makala za kishia?au kutafsiri makala hizo bila ya kua na hatimiliki?, Kama tatizo ni hati miliki nitajitahid kujua ni njia gan hasa napaswa niifate, na kama tatizo ni kutafsiri makala za kishia tu, Hilo ndilo lengo langu kwakua hakuna yeyote anayeuelezea ushia Kwa lugha ya kiswahili katika wikipedia, na hiyo en- wikipedia ninavyoifaham mimi ni wikipedia ya kiingereza nitaweka vipi makala za kiswahili? NAMI lengo langu ni kueleza ushia Kwa kiswahili?!! Naomba msaada hapo 41.222.181.212 20:19, 23 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
Ndugu, tafadhali, kabla ya mimi kupitia kurasa zako, ondoa maneno ya sifa katima mabano kwa kuwa katika Wikipedia hayatakiwi. Siwezi kupoteza muda mwingi kila mara kuyaondoa mwenyewe. Hii si kamusi elezo ya Kiislamu wala ya Kishia, wala ya Kikristo. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 09:46, 30 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
mbona Mimi sijaona hayo makatazo nimesoma Sheria za wikipedia sijaona hizo unazosema. Katika uislam kumtaja mtume ni lazima kumtakia rehma na amani . Hizo si sifa tu Bali ni wajibu kufanya hivo . 41.222.180.167 10:19, 30 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
Wikipedia zote hayo maneno ya mabano yapo,hii ya kiswaahili ndio iwe shida, au Kuna mada maalum zinazotakiwa humu na nyingine hazitakiwi? Nenda moja kwa moja kwenye tatizo,shida ni Nini? 41.222.180.167 10:23, 30 Desemba 2021 (UTC)[jibu]
Ndugu, niliwahi kukushukuru kwa kutunga makala juu ya Uislamu wa Kishia, na nilijitahidi kuziboresha, hivyo usifikiri kuna mada zinazotakiwa au zisizotakiwa, ila namna ya kuziandika isiwe ya kidini. Sijui kama kweli Wikipedia zote zina hayo maneno ya mabano ambayo ni ya kiibada, si ya kielimu. Tazama kwa mfano https://en.wikipedia.org/wiki/Muhammad --Riccardo Riccioni (majadiliano) 11:29, 30 Desemba 2021 (UTC)[jibu]

Ukiangalia enwikipedia, ile "PBUH" inapatikana kama sehemu ya nukuu, kamwe katika matini.Kwetu iwe hiyo. Kipala (majadiliano) 15:47, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]

Ndugu, ukurasa juu ya mtu huyo ulikuweko tayari, hivyo nimeondoa maandishi mapya ulioyatunga wewe. Ila ukipenda unaweza kutumia sehemu zake mbalimbali kuongezea ukurasa uliotangulia kuandikwa. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:20, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]

Nilisearch sikuuona, upo Kwa jina Gani niangalie!,, Alafu samahani sijatunga!!!ukitaka original page fuata link hyo ya chini hapo 41.222.181.36 12:35, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]
Halafu naomba kujua ni makala zenye malengo Gani hasa ambazo zinatakiwa kuwekwa wikipedia ya kiswahili? Hii ni mara ya pili nauliza sijawahi jibiwa. Je kwakua Kuna nafasi ya kuhariri makala za wikipedia ndio lazima mtu ahariri kila kitu ndani ya makala hiyo Hadi kichwa cha makala, hamuoni kufanya hivi ni kupoteza lengo la aliyeiweka makala hiyo? Kwani kama unaona mtu kaweka kitu si cha ukweli si uandike makala nyingine page tofauti Ili kumpinga, au Kuna mawazo Fulani ndyo yanayotakiwa na mengine hayatakiwi hata Kama ni ya kweli? Ninavyojua lengo mojawapo la wikipedia ni kuelimisha ,je watu wataelimikaje Kwa mawazo ya aina moja tu kila siku? naimba kwenye swali nijibiwe ,labda mi mgeni sijui🤷 Muzney Muhammad (majadiliano) 14:24, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]
Angalia vizuri kwa tahajia ya hapo juu. Utaona tuliwahi kuandika juu ya mtu huyo kabla yako. Kwanza usome kilichoandikwa, halafu utaweza kusema kama ni sawa au siyo. Inaonekana wewe huamini nia yetu ya kutosimama upande wowote. Basi, kama ukiona kilichoandikwa si sahihi au hakitoshi unaweza kuhariri au kuongezea kama nilivyokuambia. Ila usiweke msimamo wako au wa Shia tu. Jitahidi kuandika kilicho sahihi hata kama ni tofauti na mawazo yako... --Riccardo Riccioni (majadiliano) 14:38, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]
hiyo Sheria ya kutosimama upande wowote ni ya wikipedia au ni ya wahariri,wewe haujahariri ila umefuta ,kwani zikiwa makala zaidi ya moja zikielezea kitu kimoja Kwa namnatofaut Nini kinaharibika?kumbuka sizungumzii makala hii tu. 41.222.181.36 14:42, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]
Mimi hiyo niliona ila sikurdhika nayo kwasababu zipo baadhi ya taarifa za uongo na ndiomana nikaitafuta ya wairani wenyewe nikaiweka kiswahili Kwa wataohitajia,wewe hapo hata ningeihariri hiyo kwakua huamin ninachoamini ungeifuta kama ulivyoifuta niliyoandika Mimi,kwa mfano kama kweli lengo ni kuhariri mbona kuna paragrafu nyingi tu hazipo hapo,umezitoa.
Na hiyo Sheria ya kutokua upande wowote Mimi kwa mfano namzungumzia mtume Muhammad we unafkiria nitamzungumzia kulingana na wasio waislam wanavyoamini,Mimi najua wao wanamuamini vipi? Lazima nitaandika ninavyovijua kwahiyo Kwa mtazamo wako nitakua nimependelea uislam au sio??naomba nifafanulie vizur hiyo Sheria na unielekeze naipata wap kweny hii wikipedia ya kiswahili. Shukran 41.222.181.36 14:49, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]
Hivyo ukurasa huo ulikuwa umeuona, kumbe ulisema hukuuona hata kwa Google! Mimi sikufuta ukurasa wako, ila nimeuelekeza kwenye ule uliopo tangu awali, nikakuambia unaweza kutumia maandishi yako kuuongezea au kurekebisha. Kumbe wewe unataka tu kuandika sawa na Wiki ya Shia. Uwaombe wahusika wakukubalie uanzishe Wiki hiyohiyo kwa Kiswahili. Wikipedia si ya Kiislamu wala ya Kikristo. Tunapaswa kujitahidi sote kutosimama upande wetu, lakini wewe hutaki. Pole sana. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 15:02, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]
Qassim Wala si wa waislam tu Wala si wa washia tu na Wala sikumuelezea Kwa upande wa dini hapo. Tangu mwanzoni ulisema kua ukurasa upo na umeondoa maneno yangu niliyotunga mimi!!sasa umeondoa maneno niliyotunga au umereplace ukurasa wangu na huo uliokuwepo awali? Kama ilkua ni kujazia mule ungenambia moja kwa moja tangu mwanzo kama ilivyokua awali ulivyokua unanielekeza jinsi ya kutafsiri na usingenishutumi Kwa kutunga. Be specific,what Is your point . 41.222.181.36 15:24, 3 Januari 2022 (UTC)[jibu]
Ndugu, nakiri tunashindwa kuelewana. Naomba uwasiliane zaidi na kiongozi wa juu, Kipala. Amani kwako! --Riccardo Riccioni (majadiliano) 12:42, 4 Januari 2022 (UTC)[jibu]

Kaka hujambo, hal-e shoma khub-e? Al-an Iran hastid au Tanzania bar girid? Basi Riccardo aliniomba nikujibu. Ukiwa na wasiwasi kuhusu makala fulani njia inayotakiwa (haswa ukiwa mgeni) ni kupeleka maoni, maswali na ukosoaji a) kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala na b) kuyanakili (kwa heshima) kwenye ukurasa wa mtungiaji wa awali. Haitakiwi na haukubaliki kutunga makala ya pili tu. Ukiwa na maswali au maoni zaidi, karibu sana! Kipala (majadiliano) 20:24, 4 Januari 2022 (UTC)[jibu]

Kuhusu swali lako hapo juu ona: Wikipedia:Msimamo wa kutopendelea upande. Uliwahi kukumbushwa kuhusu utaratibu huo katika "karibu" iliyokufikia mwanzoni, maana hapa kuna sehemu ya Wikipedia:Mwongozo_(Kumbuka) unayotakiwa kuzingatia. Karibu sana!! Khosh amadid! Kipala (majadiliano) 20:33, 4 Januari 2022 (UTC)[jibu]