Lava Lava (mwimbaji)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Lavalava (mwanamuziki))
Lava Lava
Taarifa za awali
Jina la kuzaliwaAbdul Juma Idd
Amezaliwa(1993-03-27)Machi 27, 1993 (umri 30 )
Kazi yake

Abdul Juma Idd (maarufu kwa jina lake la kisanii Lava Lava[1]; amezaliwa 27 Machi 1993) ni mwimbaji anayetokea Tanzania aliyesajiliwa chini ya lebo ya muziki WCB Wasafi[2][3] inayomiliki wasanii wengine kama Rayvanny, Queen Darleen,Zuchu,Mbosso na Diamond Platnumz ambaye ndiye bosi wa lebo hiyo.

Lavalava ni miongoni mwa vijana wanaofanya vyema kwenye muziki wa Bongo Fleva kwa sasa. Alijiunga WCB mwaka 2015 lakini alijulikana rasmi 22 Mei 2017.

Maisha ya muziki[hariri | hariri chanzo]

Safari yake ya muziki ilianzia mtaani kwao, Bunju, Dar es Salaam ambapo alijenga jina lake kwa kuimba nyimbo za watu kiasi kwamba asipokuwepo mtaani hapo pengo lake huonekana.

Lavalava alitoroka shule na kwenda Tanzania House of Talents (kifupi: THT) kwa ajili ya kuimba, baada ya kupita kwenye mchujo wa wasanii wachanga zaidi ya 1000 na kuingia 50 bora, alifanya mafunzo ya muziki kwa miaka mitano na kukabidhiwa cheti cha masuala ya muziki na kupewa ruhusa ya kuingia mtaani kusaka au kutafuta menejimenti.

Baada ya kumaliza masomo yake aliomba nafasi WCB Wasafi na kubahatika kusajiliwa.[4]

Diskografia[hariri | hariri chanzo]

Albamu

  • Promise

Nyimbo

  • Saula akishirikiana na Harmonize
  • Warembo akishirikiana na Susumila
  • Niue
  • Gundu
  • Teja
  • Tuachane
  • Habibi
  • Jibebe akishirikiana na Mbosso na Diamond Platnumz
  • Hatuachani
  • Tukaze Roho
  • Utatulia
  • Utanipenda cover
  • Go gaga
  • Wanga
  • Tekenya
  • Corona
  • Bachela
  • Single
  • Nimekuchagua
  • Dede
  • Tattoo
  • Balaa
  • Ya Ramadhan
  • Kizungu zungu
  • Dondosa

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Lava Lava (mwimbaji) kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.