Krete

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bandari ya Heraklion.

Krete (kwa Kigiriki Κρήτη, Kríti, matamshi ya kale, Krḗtē) ni kisiwa kikuu na chenye watu wengi zaidi cha Ugiriki, na ni cha tano katika Bahari ya Kati, baada ya Sicily, Sardinia, Cyprus na Corsica.

Pamoja na visiwa vya jirani vya bahari ya Aegean kinaunda mkoa wa Krete (Περιφέρεια Κρήτης), mmoja kati ya 13 ya nchi nzima. Mwaka 2011, mkoa huo ulikuwa na wakazi 623,065.

Mji mkuu na mji mkubwa ni Heraklion.

Krete ni sehemu muhimu ya ustaarabu na uchumi wa Ugiriki ukidumisha upekee wake katika utamaduni (kwa mfano upande wa ushairi na muziki).

Historia[hariri | hariri chanzo]

Zamani (27001420 KK hivi) Krete ilikuwa kiini cha ustaarabu wa Minoa, wa kwanza kustawi huko Ulaya.[1]

Inatajwa na Biblia[2] pamoja na tabia za wakazi wake.

Katika miaka ya 60 Mtume Paulo alimuacha huko askofu Tito ili aweke wakfu mapadri katika kila mji. Halafu alimuandikia barua maarufu.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Ancient Crete Archived 30 Mei 2020 at the Wayback Machine. Oxford Bibliographies Online: Classics
  2. Mdo. 27,13

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

  • Panagiotakis, Nikolaos M. (1987). "Εισαγωγικό Σημείωμα ("Introduction")". In Panagiotakis, Nikolaos M. Crete, History and Civilization (in Greek) I. Vikelea Library, Association of Regional Associations of Regional Municipalities. pp. XI–XX. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Ugiriki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Krete kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.