Klodolfi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Klodolfi (pia: Chlodulf, Clodulphe, Clodould, Clou, Cloud; 605 - 697 hivi) alikuwa askofu wa 30 wa Metz (leo nchini Ufaransa) kwa miaka 40 hivi hadi kufikia umri wa miaka 91[1].

Baba yake, Arnulfo wa Metz, alitangulia kuwa askofu wa huko, baada ya kuachana na mke wake, Doda, ili yeye aingie upadri na mke umonaki. Kama baba yake, alikuwa pia mshauri wa mfalme wa Austrasia.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Juni[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.