Keremkerem

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Keremkerem
Kerem kidari-marungi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Coraciiformes (Ndege kama viogajivu)
Familia: Meropidae (Ndege walio na mnasaba na keremkerem)
Jenasi: Meropogon Bonaparte, 1850

Merops Linnaeus, 1758
Nyctyornis Jardine & Selby, 1830

Spishi: Angalia katiba

Keremkerem ni ndege wa familia ya Meropidae. Wana mwili mwembamba wa rangi maridadi. Mdomo wao ni mrefu na mwembamba na mkia wa aina nyingi za keremkerem una mileli mirefu katikati.

Ndege hao wanaishi uwandani kwa kanda ya tropiki na nusu-tropiki ya Afrika, Ulaya na Asia. Hula wadudu, nyuki, manyigu na mabunzi hasa, ambao wanakamatwa hewani. Kabla ya kula, ndege anatoa mshale wa mdudu akimgongea tawi la mti au kitu kigumu kingine.

Keremkerem hupenda kuwa pamoja kwa makundi. Huchimba mashimo ndani ya kando za mchanga kwa kutaga mayai yao meupe.

Familia ya Meropidae imegawika katika nusufamilia mbili: Nyctyornithinae (keremkerem wenye ndevu) na Meropinae (keremkerem wa kawaida).

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za Asia[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]