Nyigu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyigu
Dondora (nyigu mkubwa) (Vespa orientalis)
Dondora (nyigu mkubwa) (Vespa orientalis)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Hymenoptera (Wadudu wenye mabawa mangavu)
Nusuoda: Apocrita (Hymenoptera wenye kiuno chembamba sana)
Gerstâcker, 1867
Ngazi za chini

Makundi bila tabaka (2) na familia za juu (14):

  • Aculeata
    • Apoidea
    • Chrysidoidea
    • Vespoidea
  • Parasitica
    • Ceraphronoidea
    • Chalcidoidea
    • Cynipoidea
    • Evanioidea
    • Ichneumonoidea
    • Megalyroidea
    • Mymarommatoidea
    • Platygastroidea
    • Proctotrupoidea
    • Stephanoidea
    • Trigonaloidea

Nyigu wa kweli ni wadudu wa nusuoda Apocrita katika oda Hymenoptera walio na kiuno chembamba sana na kutokuwa nyuki au sisimizi. Spishi za nusuoda nyingine, Symphyta, huitwa nyigu-msumeno na hazina kiuno chembamba. Nyigu wa kweli wote ni mbuai au vidusia lakini ni lava tu ambao hula mawindo au mwathirika. Nyigu wapevu hula mbochi, mbelewele au vitu vingine vyenye sukari. Nyigu mbuai hukamata wadudu (viwavi mara nyingi) au arithropodi wengine. Huwaweka katika tundu ardhini au katika muundo wa matope au katika sega la “karatasi” baada ya kuwapooza kwa sumu katika ganglioni kuu. Halafu nyigu hulitaga yai juu ya mdudu aliyekamatwa. Huyu aendelea kuwa hai na kwa hivyo lava wa nyigu akitoka kwenye yai anapata chakula kisichooza. Hata mdudu bila bahati afa tu akiwa ameliwa takriban kabisa. Jambo la nyigu vidusia linafanana lakini nyigu hawa huacha mwathirika ambapo alimpata. Hutaga yai au mayai juu au ndani yake na lava wakitoka kwenye mayai wanaanza kula mwathirika. Kwa sababu ya mwenendo huu nyigu vidusia hutumika sana kwa kufanya udhibiti wa kibiolojia dhidi ya visumbufu.

Kinyume na nyigu wengine spishi za familia Chalcidae (nyigu-kidutu) husababisha vidutu kwa majani ya mimea na lava hula tishu yao. Spishi jamaa za familia Agaonidae (nyigu-makuyu) huyataga mayai yao katika ovari za maua ya mikuyu.

Kuna majina mbalimbali kwa makundi ya nyigu, kama vile: bunzi, dondora, mavu, nyigu-kidutu, nyigu-makuyu na uvi.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyigu kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.