Kachori

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kachori ni vitafunio vya kukaanga sana, vinavyotokana na viazi mbatata ambavyo vimechemshwa na kupondwapondwa, kisha vimetiwa viungo mbalimbali, kama chumvi, ndimu na pilipili; hatimaye vikakaangwa kwa mafuta.

Asili yake ni Bara Hindi, na hujulikana katika maeneo na diaspora ya India na maeneo mengine ya Asia Kusini.

Kachori zilikuwa maarufu katika Indore ya zamani, hata kabla ya samosa kupata umaarufu baada ya kugawanywa kwa India. [1]

Banarasidas, mwandishi wa wasifu Ardhakathanaka, ametaja kununua kachori huko Indore mnamo 1613. [2] Kwa miezi saba, alinunua kachori kila siku, na alikuwa na deni la rupia ishirini. [3]

Inasemekana kachori imeanzia Uttar Pradesh, India.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Samosas from Sindh, kachoris from Old Delhi, R. V. SMITH, The Hindu, January 30, 2016
  2. Banarasidas, Ardha-Kathanaka, verses 335-342
  3. Nathuram Premi, Kavivar Banarsidas viracit Ardha Kathanaka, Bombay, Hindi Granth Ratnakar, 1957
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kachori kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.