Irene Tarimo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Daktari
Irene Tarimo
Mhadhiri
Amezaliwa1 Oktoba 1964 (1964-10-01) (umri 59)
UtaifaMtanzania
Majina mengineIrene Aurelia Tarimo
ElimuSekondari ya Kilakala
Sekondari ya Weruweru
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
Kazi yakeMhadhiri na Mtafiti Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
MwenzaIsdory Tarimo (m. 1992–present) «start: (1992)»"Marriage: Isdory Tarimo to Irene Tarimo" Location: (linkback://sw.wikipedia.org/wiki/Irene_Tarimo)
NduguJohn Mrosso

Irene Aurelia Tarimo (alizaliwa mwaka 1964) ni mhadhiri nchini Tanzania, na Mkuu wa Idara ya Masomo ya Sayansi ya Mazingira katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania [1]. Pia ni mwanasayansi na mtafiti katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania [2]. Alikuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Mkoa wa Lindi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa takribani miaka kumi.[3]

Wasifu

Irene alimaliza elimu yake ya awali ya msingi Rombo. Katika elimu yake ya sekondari alikuwa mwanafunzi katika shule ya wasichana ya Weruweru iliyopo mjini Kilimanjaro na baadae kujiunga kidato cha tano na sita na shule ya wasichana ya Kilakala iliyopo Morogoro. Alijiunga na Chuo cha Uwalimu cha Dar es Salaam (DUCE) na kusoma masomo ya Kemia, Biolojia na Taaluma. Alipomaliza alipata ajira ya uwalimu katika shule za sekorandari, Shule ya Sekondari ya Kifungilo, Shule ya Sekondari ya Morogoro, Shule ya Sekondari ya Weruweru na Shule ya Sekondari ya Mwika.

Mwaka 1995 alijiunga Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na mwaka 2003 alitunukiwa Shahada ya awali ya Sayansi katika Taaluma (B.Sc.Ed) kwa daraja la kwanza. Irene aliweka historia kwa kuwa mwanafunzi wa kwanza tangu miaka kumi ya kuanzishwa Chuo Kikuu Huria mwaka 1992 kupata Alama ya daraja la kwanza. Alipata zawadi kutuka kwa Makamo Mkuu wa chuo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Irene alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa masomo ya Shahada ya pili ya Uzamili katika Sayansi ya Mazingira na kuhitimu mwaka 2007. Baadaye alijiunga tena na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa Shahada ya tatu ya Uzamivu akishirikiana na Chuo Kikuu cha Copenhagen mpaka kumaliza kwake mwaka 2013.

Kazi

Daktari Irene amekuwa Mkurugenzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Mkoa wa Lindi kwa takribani miaka tisa tangu 2007 amewezesha shughuli za chuo ukanda wa Mikoa ya kusini mwa Tanzania kufanikiwa kwa ustadi na uadilifu mkubwa.[4] Amewezesha kituo cha Lindi kupata eneo la Ardhi takribani Ekari 100 kwa ajili ya upanuzi wa ujenzi wa makazi mapya ya kituo cha chuo. Pia alifanikisha upatikanaji wa Ekari takribani 3 kwa ajili ya maonyesho ya Nane Nane eneo la Ngongo, Mkoani Lindi [5]. Alifanikisha harambee ya upatikanaji gari la usafiri wa chuo na kwa shughuli nyingine mbalimbali za chuo [6].

Dkt. Irene Tarimo na Salma Kikwete kwenye mahafali

 

Machapisho

Irene Aurelia Tarimo ameandika machapisho kadhaa juu ya Sayansi na mambo ya kijamii:

Marejeo

  1. "Mkurugenzi Ndaki ya Sayansi na Mazingira". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-10-31. Iliwekwa mnamo 2020-07-14. 
  2. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-03-13. Iliwekwa mnamo 2020-07-11. 
  3. Huria cha Tanzania, Chuo Kikuu [@Open_univ_tz] (8 Machi 2022). "Siku ya Wanawake Duniani 2022, Dr. Irene Tarimo anasema...!" (Tweet). Iliwekwa mnamo 2 Mei 2023 – kutoka Twitter. 
  4. Vijana someni ili mnufaike na gesi na mafuta
  5. Mamlaka ya Mkoa wa Lindi yatoa ardhi CKHT
  6. Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yafanikisha Harambee
Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Irene Tarimo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: