Hunfridi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Hunfridi, OSB (alifariki Therouanne, Ufaransa wa leo, 871) alikuwa mmonaki aliyechaguliwa mwaka 856 kuwa askofu wa mji huo ingawa hakupenda.

Hali ilikuwa ngumu sana upande wa siasa, kutokana na uvamizi wa Wanormani walioteketeza mji, na upande wa Kanisa vilevile, kutokana na maadili kumomonyoka kabisa hata utawani.

Papa Nikola I alimhimiza aendelee na kazi yake, naye akakubali akawa faraja ya wananchi hadi kifo chake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Machi[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.