Kitaumande

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Glaucidium)
Kitaumande
Kitaumande miraba
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Strigiformes (Ndege kama bundi)
Familia: Strigidae (Ndege walio na mnasaba na bundi)
Nusufamilia: Surniinae (Ndege walio na mnasaba na bundi-panga)
Jenasi: Aegolius Kaup, 1829

Athene Boie, 1822
Glaucidium Boie, 1826
Micrathene Coues, 1866
Xenoglaux O'Neill & G.R. Graves, 1977

Spishi: Angalia matini

Vitaumande ni ndege mbuai wa jenasi mbalimbali wa nusufamilia Surniinae katika familia Strigidae. Ndege hawa ni wadogo kuliko bundi (sm 12-28) na wana rangi ya kahawa au kijivu pamoja na miraba au madoa.

Vitaumande hula panya na wanyama na ndege wadogo wengine na hata watambaazi wadogo, popo, samaki, wadudu na nyungunyungu. Kulingana na spishi huwinda wakati wa alasiri au alfajiri au hata mchana na pengine usiku.

Jike huyataga mayai 2-7 katika tundu lililoachwa na ndege au mnyama mwingine, mara nyingi lile la kigong'ota au zuakulu. Spishi fulani huchimba vishimo katika ardhi au nyingine hutaga ndani ya matundu katika miamba, kingo za mito au majengo makuukuu au hata ndani ya vishimo vya sungura.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Spishi za kabla ya historia[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]