Epikur

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Epicurus)
Sanamu ya Kirumi ya Epicurus.

Epikur (kwa Kilatini na lugha mbalimbali Epicurus, kutoka Kigiriki Ἐπίκουρος, Epíkouros, yaani "Mwenzi"; 341270 KK) alikuwa mwanafalsafa wa Ugiriki wa Kale, maarufu kama mwanzilishi wa shule ya falsafa yenye jina lake (kwa Kiingereza: Epicureanism).

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

Kati ya maandishi yake 300 hivi, zimebaki tu sehemu na barua chache; zaidi tunajua kutoka kwa wafuasi wake na wengineo waliofafanua mafundisho yake.

Mafundisho[hariri | hariri chanzo]

Kwake, lengo la falsafa ni kufikia maisha yenye heri, utulivu, amani, kutoogopa, kutoteseka, kujitegemea na kuzungukwa na marafiki. Kwake raha na maumivu ndio vigezo vya uadilifu au uovu wa mambo yoyote. Pia kifo ni mwisho wa mwili na roho, hivyo hakitakiwi kuogopwa. Tena hakuna miungu ambao waadhibu wala kutuza binadamu. Ulimwengu hauna mipaka na ni wa milele.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake
Ufafanuzi

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Sura
Vyanzo
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Epikur kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.