Dorotheo wa Turo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Dorotheo wa Turo (Antiokia ya Siria, leo nchini Uturuki, 255 hivi - Varna, Bulgaria, 362) alikuwa askofu wa mji huo wa Lebanoni [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 5 Juni[2][3].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Dhuluma ya kaisari Diocletian ilimlazimisha kukimbia alipokuwa padri maarufu kwa elimu yake, lakini baadaye akarudi.

Alishiriki mtaguso wa kwanza wa Nisea mwaka 325, lakini alifukuzwa na kaisari Juliani Mwasi akakae Odyssopolis (Varna, leo nchini Bulgaria) kwenye Bahari Nyeusi. Huko alifia dini yake akiwa na umri wa miaka 107.

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

Anasemekana kuwa mwandishi wa "Matendo ya Wanafunzi Sabini" waliotumwa na Yesu kadiri ya Injili ya Luka 10:1.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Eusebius,VII.32
  2. Martyrologium Romanum
  3. Saint Dorotheus of Tyre. Saints.SQPN. Iliwekwa mnamo April 5, 2011.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Christian cross.svg Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.