Daudi wa Thesalonike

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Daudi wa Thesalonike

Picha takatifu ya Mt. Daudi akiishi juu ya mlozi
Amezaliwa 450
Feast

Daudi wa Thesalonike (Mesopotamia, 450 hivi - Thermes, Ugiriki, 540) alikuwa mmonaki aliyepata umaarufu kwa karama yake ya ushauri iliyomvutia heshima ya wanajumuia wenzake na ya umati wa watu.

Walipotaka kumfanya abati, baada ya kuishi miaka 80 katika chumba kidogo nje ya mji, alikataa akaenda kuishi miaka 3 juu ya mti wa mlozi[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi, Wakatoliki na Waanglikana kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Juni[2][3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Parry, Ken (1999). David Melling, mhariri. The Blackwell Dictionary of Eastern Christianity. Malden, MA.: Blackwell Publishing. ISBN 0-631-23203-6. 
  • Velimirovic, Nicholas. The Prologue from Ochrid, vol. 2. Birmingham: Lazarica Press, 1986

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.