Alberto wa Yerusalemu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake huko Milano.

Alberto wa Yerusalemu (alizaliwa Castel Gualtieri, Italia, karne ya 12 - alifariki Akka, Israeli, 14 Septemba 1214) alikuwa kwanza kanoni, halafu askofu wa Bobbio, halafu wa Vercelli nchini Italia, halafu tena wa Yerusalemu katika Nchi Takatifu[1].

Ndiye aliyewapa kanuni watawa Wakarmeli. Aliuawa kwa upanga na mtu aliyekuwa amemlaumu na kumshusha cheo.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.