Éder Militão

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Éder Militão

Eder Gabriel Militão (alizaliwa Sertãozinho, São Paulo, Brazili, 18 Januari 1998) ni mchezaji wa soka wa Brazili ambaye anacheza kama beki wa kati au kiungo mkabaji wa klabu ya Real Madrid.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Militão alianza kucheza mpira wa miguu na vijana wa São Paulo mwaka 2010.

Alikuwa beki bora katika timu ya kwanza ya 2016 Copa Paulista.

Tarehe 7 Agosti 2018, Militão alisaini mkataba wa miaka mitano na mabingwa wa Ureno FC Porto. Alicheza mechi ya kwanza na Porto mnamo 2 Septemba, akianza na ushindi wa nyumbani wa 3-0. Yeye alisababisha magoli mawili kwa Héctor Herrera.

Mwaka wa 2019 alinunuliwa na klabu ya Real Madrid.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Éder Militão kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.