Yosefu Maria Robles

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Yosefu Maria.

Yosefu Maria Robles (kwa Kihispania José Maria Robles Hurtado, Mascota, Jalisco, Mexico, 3 Mei 1888 - Quila, Jalisco, 26 Juni 1927) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki nchini Meksiko hadi alipouawa kwa kutundikwa mtini bila kesi wakati wa Vita vya Wakristero.

Kwa miaka 14 alikuwa amehudumia kwa upendo mkubwa waamini wake, pamoja na kuandika vitabu vya Kikristo na kuanzisha shirika la Masista wa Moyo Mtakatifu wa Yesu[1].

Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri tarehe 22 Novemba 1992 halafu mtakatifu mfiadini tarehe 21 Mei 2000 pamoja na wenzake 24 waliofia dini katika vita hivyo[2]:

Sikukuu yao inaadhimishwa kila tarehe 21 Mei ila ya kwake mwenyewe ni tarehe ya kifodini chake[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.