Yohane Maria Vianney
Yohane Baptista Maria Vianney (Dardilly, 8 Mei 1786 – Ars-sur-Formans, 4 Agosti 1859), alikuwa padri mwanajimbo wa Kanisa Katoliki kutoka Ufaransa; kwa miaka mingi alifanya kazi ya uchungaji kama paroko wa kijiji cha Ars, huku sifa zake zikivuta watu kutoka nchi za nje ya Ulaya pia.
Alitangazwa na Papa Pius X kuwa mwenye heri tarehe 8 Januari 1905, halafu Papa Pius XI akamtangaza mtakatifu mwaka 1925 na msimamizi wa maparoko mwaka 1929.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].
Sala zake[hariri | hariri chanzo]
Nakupenda, Bwana, na neema pekee ninayokuomba, ni kwamba nikupende milele...
Mungu wangu, ikiwa ulimi wangu hauwezi kukariri kila nukta kwamba nakupenda, nataka moyo wangu ukuambie tena na tena kila ninapopumua.
Yesu wangu, jinsi inavyopendeza kukupenda!
Unijalie niwe kama wanafunzi wako juu ya mlima Tabori, nikikuona wewe tu, Mwokozi wangu.
Tuwe kama marafiki wawili ambao hata mmojawao hawezi kukubali kumchukiza mwingine. Amina.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- John Vianney--Cure d'Ars Archived 17 Februari 2011 at the Wayback Machine.
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |