Saint-Denis (Reunion)
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Saint-Denis | |
| Nchi | Réunion |
|---|---|
Saint-Denis (au Saint-Denis de la Réunion) ni mji mkuu wa eneo la ng’ambo la Ufaransa (yajulikana kwa Kifaransa kama "département d'outre-mer") la Réunion ambayo ni kisiwa kimoja cha funguvisiwa ya Maskarena katika Bahari Hindi.
Saint-Denis ni pia mji mkubwa wa kisiwa ikiwa na wakazi 131,557 (mwaka 1999).
Historia [hariri]
Saint-Denis ilianzishwa na Mfaransa Étienne Régnault mnamo mwaka 1669 ikawa mji mkuu wa kisiwa mwaka 1738.
Usafiri [hariri]
Kuna kiwanja cha ndege cha Aéroport de la Réunion Roland Garros ambayo ni geti ya kisiwa kwa safari za kimatifa. Bandari kuu ya kisiwa iko Pointe-des-Galets nje ya mji.
Viungo vya nje [hariri]
- Ukurasa rasmi wa mji (Kifaransa)