Funguvisiwa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Funguvisiwa la Galapagos katika Pasifiki

Funguvisiwa ni kundi la visiwa vinavyokaa sehemu pamoja baharini. Mara nyingi kundi la namna hiyo lina asili moja, kama vile kuwa mabaki ya kisiwa kikubwa zaidi kilichogawika kutokana na mmomonyoko wa ardhi yake au kuwa na asili ya volkeno.

Atolli inaweza kuonekana pia kama kundi la visiwa lakini huhesabiwa zaidi kama kisiwa kimoja hata kama sehemu kadhaa ziko chini ya maji. Katika Bahari ya Pasifiki na Bahari Hindi kuna mafunguvisiwa ya atolli.

Funguvisiwa kubwa kabisa duniani ni lile la Indonesia pamoja na Ufilipino linaloitwa pia Funguvisiwa la Malay.

Bahari ya Pasifiki ina mafunguvisiwa mengi, pia sehemu ya Karibi ya Bahari ya Atlantiki karibu na Amerika ya Kati.

Mafunguvisiwa muhimu ya Afrika ni Zanzibar, Shelisheli na Komoro katika Bahari Hindi, halafu Visiwa vya Kanari na Visiwa vya Madeira katika Atlantiki.

Mafunguvisiwa madogo karibu na pwani ya Afrika ya Mashariki ni kama vile ya Lamu, Kilwa na Kirimba.

Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.