S

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alfabeti ya Kilatini
(kwa matumizi ya Kiswahili)
Aa Bb Cc ch Dd
Ee Ff Gg Hh Ii Jj
Kk Ll Mm Nn Oo Pp
Qq Rr Ss Tt Uu Vv
Ww Xx Yy Zz

S ni herufi ya 19 katika alfabeti ya Kilatini ambayo ni pia mwandiko wa Kiswahili cha kisasa. Asili yake ni Sigma ya alfabeti ya Kigiriki.

Maana za S[hariri | hariri chanzo]

Historia ya S[hariri | hariri chanzo]

Kisemiti asilia
alama ya meno
Kifinisia
shin
Kigiriki
Sigma
Kietruski
S
Kilatini
S

Asili ya herufi S ni miandiko iliyotangulia alfabeti ya Kilatini. Waroma walipokea mwandiko kutoka alfabeti ya Kigiriki kupitia alfabeti za Kiitalia za awali kama Kietruski. Wagiriki walipokea kutoka Wafinisia.

Wafinisia walikuwa na alama ya "shin" iliyokuwa kiasili picha iliyorahisishwa ya meno wakitumia alama tu kwa sauti ya "sh" na kuiita kwa neno lao kwa meno "shin". Wagiriki walichukua alama hiyo na kuiita "sigma" bila kujali maana asilia ya "meno". Kwao imekuwa sauti tu ya "s" kwa sababu hawakujua "sh".

Waitalia wa kale kama Waetruski wakapokea herufi wakigeuza mwelekeo wake. Waroma wakaichukua kutoka hapa lakini walilainisha kona kali kuwa S jinsi ilivyo hadi sasa.