L
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Alfabeti ya Kilatini | ||||||
|---|---|---|---|---|---|---|
| Aa | Bb | Cc | ch | Dd | ||
| Ee | Ff | Gg | Hh | Ii | Jj | |
| Kk | Ll | Mm | Nn | Oo | Pp | |
| Rr | Ss | Tt | Uu | Vv | ||
| Ww | Xx | Yy | Zz | |||
L ni herufi ya 12 katika alfabeti ya Kilatini ambayo ni pia mwandiko wa Kiswahili cha kisasa. Asili yake ni Lambda ya alfabeti ya Kigiriki.
[hariri] Maana za L
- Kwa magari L ni alama ya gari kutoka Luxemburg.
- kati ya namba za Kiroma "L" ni alama ya namba 50
[hariri] Historia ya L
| Kisemiti asilia Fimbo la kuchungia ng'ombe |
Kifinisia Lamed |
Kigiriki Lambda |
Kietruski L |
Kilatini L |
|---|---|---|---|---|
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
Asili ya alama ni picha andishi iliyoonyesha fimbo la kuchungia ng'ombe. Wafinisia walirahisihsa alama hiyo na kuiita kwa neno lao la fimbo hili "lamed". Wakaitumia kama alama ya sauti "l". Wagiriki wa Kale wakaipokea kama "Lambda" na kubadilisha umbo lake kuwa kama paa ya nyumba.
Waetruski walipendelea umbo la kifinisia kwa kuiandika kama alama ya sauti "l". Waroma wa Kale wakageuza alama na kunyosha mikono yake kuwa L jinsi iliovyo hadi leo.
| Makala hiyo kuhusu "L" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu L kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |



