Raphael
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Raffaello Sanzio (ajulikana kama Raffael au Raphael) (6 Aprili 1483 - 6 Aprili 1520) alikuwa mchoraji na mjenzi kutoka Italia. Pamoja na Leonardo da Vinci na Michelangelo huhesabiwa kati ya wasanii muhimu wa zama ya mwamko ya Italia. Alizaliwa mjini Urbino kwa hiyo huitwa pia Raffaello da Urbino au Raffaello Sanzio de Urbino.
[hariri] Maisha
Raphael alizaliwa kama mtoto wa mchoraji Giovanni Santi aliyefanya kazi katika utumishi wa mkabaila Frederiko III wa Montefeltro.
Kwa umri wa miaka 15 alikuwa mwanafunzi katika karakana ya mchoraji Pietro Perugino aliyeshiriki katika kazi za kupamba kanisa la Sistina kwenye Vatikano. Raphael alijifunza haraka na tangu 1500 alipokuwa na umri wa miaka 17 alipewa kazi za kwanza za kujitegemea.
Alianza kuchora picha kwa makanisa katika miji mbalimbali ya Italia. Alipenda kutembelea Firenze akitazama michoro ya walimu wa kale.
Tangu alihamia Roma alikoitwa na Papa Julius II. Kazi kubwa aliyopewa ilikuwa picha za ukutani kwenye vyumba vya Papa mwenyewe.
Raphael aliaga dunia mapema kwa umri wa miaka 37. Hakuoa na hakuna watato waliojulikana.
[hariri] Picha za Raphael
|
Kardinali Tommaso Inghirami (1515-1516) |
|||
|
Mariamu na mtoto Yesu (mnamo 1507) |
Kristo (1507) |
||
|
Picha ya Maddalena Doni, (1506) |
Picha ya mwanamke aliyeitwa "La Muta", Galleria Nazionale delle Marche mjini Urbino |
||
|
Msalaba (1507) |
Mt. Georges apigana na joka (1505) |
||
[hariri] Viungo vya Nje
- (Kifaransa) Picha kadhaa za Rapahel
- (Kifaransa) Tovuti ya kibiashara inayoonyesha picha 275 za Raffaello Santi
- (Kiingereza) Raphael kwenye Artcyclopedia