Raphael

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Raphael alivyojichora mwenyewe

Raffaello Sanzio (ajulikana kama Raffael au Raphael) (6 Aprili 1483 - 6 Aprili 1520) alikuwa mchoraji na mjenzi kutoka Italia. Pamoja na Leonardo da Vinci na Michelangelo huhesabiwa kati ya wasanii muhimu wa zama ya mwamko ya Italia. Alizaliwa mjini Urbino kwa hiyo huitwa pia Raffaello da Urbino au Raffaello Sanzio de Urbino.

[hariri] Maisha

Raphael alizaliwa kama mtoto wa mchoraji Giovanni Santi aliyefanya kazi katika utumishi wa mkabaila Frederiko III wa Montefeltro.

Kwa umri wa miaka 15 alikuwa mwanafunzi katika karakana ya mchoraji Pietro Perugino aliyeshiriki katika kazi za kupamba kanisa la Sistina kwenye Vatikano. Raphael alijifunza haraka na tangu 1500 alipokuwa na umri wa miaka 17 alipewa kazi za kwanza za kujitegemea.

Alianza kuchora picha kwa makanisa katika miji mbalimbali ya Italia. Alipenda kutembelea Firenze akitazama michoro ya walimu wa kale.

Tangu alihamia Roma alikoitwa na Papa Julius II. Kazi kubwa aliyopewa ilikuwa picha za ukutani kwenye vyumba vya Papa mwenyewe.

Raphael aliaga dunia mapema kwa umri wa miaka 37. Hakuoa na hakuna watato waliojulikana.


[hariri] Picha za Raphael

[hariri] Viungo vya Nje