Michelangelo
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Michelangelo di Lodovico Buonarroti Simoni (6 Machi 1475 - 18 Machi 1564) alikuwa msanii nchini Italia aliye maarufu kama mchongaji, mchoraji, msanifu majengo na mshairi. Huhesabiwa kati ya wasanii muhimu zaidi wa zama ya mwamko.
Kati ya kazi zake maarufu ni sanamu ya kijana Daudi na picha za ukutani wa Kanisa la Sistina mjini Roma alilopamba kwa hadithi na watu wa Biblia.
Kati ya kazi zake maaraufu kama msanifu majengo ni hasa kubba ya Kanisa Kuu la Mt. Petro kwenye Vatikano mjini Roma.
[hariri] Picha
|
Mateso ya Mt. Petro, kanisa Paolina - Vatikano. |
Pietà (Huzuni ya Mariamu na maiti ya Yesu) ya Michelangelo Kanisa Kuu la Mt. Petro katika Vatikano. |
||
| Makala hii kuhusu mtu bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Michelangelo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |