Mbabane

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mbabane ni mji mkuu wa Eswatini


Jiji la Mbabane
Nchi Eswatini

Mbabane ni mji mkuu wa Eswatini ikiwa na wakazi 70,000 (2003). Ofisi za serikali ziko huko lakini bunge na jumba la mfalme yako mjini Lobamba.

Mji uko kwenye milima ya Mdimba kwenye kimo cha mita 1200 juu ya UB.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mji ulianzishwa na Waingereza mwaka 1902 BK baada ya vita dhidi ya makaburu ukawa makao makuu ya kiutawala ya eneo la Uswazi.

Jina limetokana na chifu Mbabane Kunene aliyekuwa mkuu wa sehemu ile wakati wa kuunda mji.

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Nguvu ya kiuchumi ya Mbabane ni migodi ya karibu ya bati na dhahabu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mbabane kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.