Yombo Vituka
Kata ya Yombo Vituka | |
Mahali pa Yombo Vituka katika Tanzania |
|
Majiranukta: 6°52′8″S 39°15′40″E / 6.86889°S 39.26111°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Mkoa | Dar es Salaam |
Wilaya | Temeke |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 59,975 |
Yombo Vituka ni jina la kata ya Wilaya ya Temeke katika Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania yenye postikodi namba 15115[1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2002, kata ina wakazi wapatao 59,975 waishio humo.[2] Yombo Vituka awali kwenye miaka ya 1980 na mwanzoni mwa miaka ya 1990 ilikuwa na eneo kubwa la mashamba ya watu ya miembe, mikorosho, mpunga, na kadhalika. Lakini kuanzia miaka ya 1995 na kuendelea, kata imeanza kupanuka kwa kiasi kikubwa sana na kupelekea kuwa na majumba mengi ya watu wenye uwezo. Leo hii, Yombo Vituka imekuwa sehemu yenye wakazi wengi kupita hata kata zake za jirani kama vile Kiwalani na Kitunda.

Marejeo
- ↑ https://www.tcra.go.tz/images/documents/postcode/dsm.pdf[dead link]
- ↑ 2002 Population and Housing Census General Report (en). Government of Tanzania. Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-02-10. Iliwekwa mnamo 2008-08-21.
![]() |
Kata za Wilaya ya Temeke - Tanzania | ![]() |
---|---|---|
Azimio | Buza | Chamazi | Chango'mbe | Charambe | Keko | Kibondemaji | Kiburugwa | Kijichi | Kilakala | Kilungule | Kurasini | Makangarawe | Mbagala | Mbagala Kuu | Mianzini | Miburani | Mtoni | Sandali | Tandika | Temeke | Toangoma | Yombo Vituka |
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Yombo Vituka kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |