Wilaya ya Biharamulo

Wilaya ya Biharamulo ni wilaya mojawapo ya Mkoa wa Kagera, Tanzania kaskazini magharibi, yenye postikodi namba 35600 [1]. Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 323,486 [2]
Wasubi, walio kundi linalohesabiwa kati ya Wanyambo, Wazinza, Wahaya na Walongo, ndio wakazi asilia wa wilaya ya Biharamulo,
Jina[hariri | hariri chanzo]
Inasemekana, asili ya jina Biharamulo ni neno la Kisubi "Niharemuno" likimaanisha "Ni mbali mno". Neno hilo lilikuwa jibu la mzee mmoja kwa Mzungu aliyemuuliza wakati wanasafiri pamoja kutoka Geita kwenda kijiji cha Nyarubungo kilichopo Biharamulo. Mzungu alimuuliza Mzee huyo, "How many kilometers from here to Nyarubungo?" yaani, "Kuna kilomita ngapi kutoka hapa kwenda Nyarubungo?" na mzee yule alijibu, "niharemuno" akimaanisha "ni mbali mno'.
Historia[hariri | hariri chanzo]
Wilaya hii pamoja na Wilaya ya Karagwe zilianzishwa na kutangazwa rasmi na Gavana wa Kiingereza Richard Turnbull mwaka 1958.
Shughuli[hariri | hariri chanzo]
Uchumi ni pamoja na ufugaji wa ng'ombe na mbuzi, kilimo cha kahawa, migomba, mihogo, mahindi, maharage na zao la pamba katika maeneo machache. Shughuli nyingine za kiuchumi katika wilaya ya Biharamulo ni uvuvi, biashara na uchimbaji madini.
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2018-08-05. Iliwekwa mnamo 2018-02-01.
- ↑ Sensa ya 2012, Kagera - Biharamulo-District-Council
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- About maternal & newborn health (MNH) in Biharamulo District Archived 4 Machi 2016 at the Wayback Machine.
- Tovuti ya BOSEDA Biharamulo originating socio - economic development association Archived 4 Machi 2016 at the Wayback Machine.
![]() |
Kata za Wilaya ya Biharamulo - Mkoa wa Kagera - Tanzania | ![]() |
---|---|---|
Biharamulo Mjini | Bisibo | Kabindi | Kalenge | Kaniha | Katahoka | Lusahunga | Nemba | Nyabusozi | Nyakahura | Nyamahanga | Nyamigogo | Nyantakara | Nyanza | Nyarubungo | Runazi | Ruziba |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kagera bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Biharamulo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno. |